بسم الله الرحمن الرحيم

kutafuta elimu ni faradhi kwa kila muislamu
الحمد لله الذي نستعينه ونستغفره ونعوذ بالله من شرور أنفسنا ومن سيئات أعمالنا من يهد الله فلا مضل له ومن يضلل فلا هادي له .



ونشهد أن لا إله إلا الله وحده لا شريك له ونشهد أن محمدا عبده ورسوله أرسله بالهدى ودين الحق ليظهره على الدين كله وكفى بالله شهيدا




Sunday, July 4, 2010

FUNZO KWA VIJANA

Allaah Atakuajiri…Tawakkal Kwake!
Kijana mmoja alimaliza kusoma katika Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Madiynatul-Munawwarah na alikuwa mfano wa pekee kwa uhodari wake na mwenye akili nyingi alimaliza na kutunukiwa Shahada yake nzuri na akiwa na vyeti vinginevyo vya mapendekezo.
Lakini akazunguka kutafuta kazi katika kila shirika, na idara za serikali bila ya kufanikiwa kupata kazi popote.
Na kwa vile alitamani na kuazimia kuwa hatotoka katika uzuri wa vizuri. Nao ni mji huu mtukufu wa Madinatul-Munawwarah, kwani je, nani anayeonja maisha mazuri kabisa katika uzuri na mazuri ya mji huu wa mpenzi (wetu Mtume صلى الله عليه وسلم ) kisha akataka kuyawacha? Naye anaona makumbusho ya Mpenzi Mustafa صلى الله عليه وسلم na Maswahaba zake رضي الله عنهم katika kila shibiri ya mji huu? Kwani alitamani kuishi Madina akitumaini na kutegemea kupata fadhila za hadithi ya Mtume صلى الله عليه وسلم aliyosema :
((Atakayeweza kufia Madinah afanye hivyo kwani mimi nitamuombea shufaa atakayefia hapo))
Akaenda kwa mmoja wa walezi wema na miongoni mwa masheikh wema ambaye anayemuona humkumbusha Allaah سبحانه وتعالى, na anayemsikia sauti yake utajua kwamba ana khofu ya Allaah سبحانه وتعالى wala haifai kumtukuza mtu isipokuwa Allaah سبحانه وتعالى .
Kasema: "Nilikwenda kwake nikamwambia "Ewe Sheikh je, humjui mtu wa kuniajiri kazi? Kwani milango imefungika mbele yangu, wala haujabakia mlango nisiougonga na yote haikufaa kitu. Wala sitaki kutoka katika mji huu wa Madiynah". Sheikh akasema kwa lafudhi yenye kujiamini “Mwenye kuwa na yakini na ahadi ya Allaah, naam Wallaahi namjua nani wa kukuajiri".
Kwa haraka kabisa nikasema (huku furaha yangu ikidhihirika). Nani huyo ewe Sheikh? Mwenyeezi Mungu Akuzidishie mema. Nani huyo? Akasema Sheikh: "Huyo ni Allaah "عز وجل
Nikapigwa na bumbuwazi!
Akanitizama Sheikh akasema : "Ajabu! Ningelikwambia kuwa ni Waziri fulani na mhusika fulani ungelifurahikiwa na kuona ni kheri. Lakini nilipokutajia Yule Ambaye Anamiliki funguo za kila kitu na Yeye ndiye Muweza wa kila kitu, Ambaye Anamiliki vyote vya mbingu na Ardhi na khazina za mbingu na ardhi, naona uso wako umebadilika kama vile kwamba una shaka na ahadi ya Allaah سبحانه وتعالى Ambaye amesema"
((وَفِي السَّمَاء رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ))
{{Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa}}
Adh-Dhariyaat 22
"Nenda ewe mwanangu kwenye msikiti wa Mtume صلى الله عليه وسلم kabla ya Alfajiri kwa saa moja umkaribie Allaah تعالى katika thuluthi ya mwisho ya usiku (katika masaa ya kabla ya Alfajiri) na mimi nina hakika na kutumainika kwamba Allaah Atakutimizia amri (haja ) yako.
Akasema (kijana): “Nilitahayari na kuona haya kabisa, tahayuri ambayo sijawahi kuihisi kabla. Nikamuaga Sheikh kisha nikaondoka"
Nikaegesha kengele ya saa yangu kuniamsha saa tisa baada ya nusu ya usiku wa manane nikamka nikatawadha, kisha nikaenda Masjidi-An-Nabawi mtukufu huku nimejaa joto la imani ambalo siwezi kulielezea.
Nilipoingia, nikaswali ilivyopasa nikataka kunyanyua mikono yangu mbinguni niombe, lakini sikuweza kwa kuzidiwa na kilio ambacho kilinizidi nguvu hata nikadhania kuwa roho yangu itatoka na huku nikiwaudhi walio karibu yangu. Nikamuomba Allaah سبحانه وتعالى maneno machache na Allaah سبحانه وتعالى ndiye Ajuaye yaliyomo vifuani.
Nikaswali Swalah ya jamaa ya Alfajiri kisha nikahudhuria darasa la mmoja wa wanachuoni wetu wenye kuheshimika kisha nikaelekea nyumbani kwangu. Nikawa nimesahau kila kitu isipokuwa Allaah سبحانه وتعالى wala sikujiandaa kufikiri au kupanga chochote katika mambo ya dunia siku hiyo
Wakati niko njiani nikahisi kama mtu akiniambia elekea njia hiyo nyingine. Nikaelekea huko, mara nikakuta ofisi ya Idara ya serikali ambayo sijawahi kabla kuipitia. Nikasema rohoni 'kwa nini nisiende nikawaulize kama wanayo kazi waniajiri?"
Nikaingia, kisha nikamkabili bwana mmoja aliyetabasamu usoni kwangu aliponiona naye wala hanijui.
Nikamuuliza: "Ewe ndugu yangu mimi simjui mtu hapa, lakini ukipenda kupata thawabu, hivi hapa vyeti vyangu na shahada zangu, hakika mimi siku nyingi natafuta kazi sijafanikiwa. Alipotazama shahada zangu akaegemea pembeni mwa maktaba yake kwa mikono yake, akainuka na kunitizama akasema: "Subhana Allaah! muda mrefu sisi tunatafuta watu wanaomiliki elimu kama hii uliyonayo, ulikuwa wapi? umekuja kutoka wapi? Sasa hivi utapata kazi Insha Allaah!"
Akasema (Kijana): 'Nikainuka kitini nikamsujudia Allaah سبحانه وتعالى sajda ya kumshukuru hapo hapo ofisini kwake huku machozi yakinilenga machoni mwangu na huku nikimkumbuka yule Sheikh mwema na yakijirudia maneno yake, “Huyo ni Allaah عز وجل , Huyo ni Allaah عز وجل"
Kisa hiki ni cha kweli. Na ingawa ni kifupi, lakini utaona kwamba kina mafundisho mengi yenye manufaa kwetu:

1. Kuwa na Tawakkul na Yakini Na Allaah سبحانه وتعالى
2. Sio hoja kusoma na kupata Shahada bali Allaah سبحانه وتعالى Ndiye Mwenye Kumruzuku mtu.
3. Kuupenda mji wa Madinatul-Munawwarah na kupata fadhila zake.
4. Ni vizuri sana kutafuta Nasiha/ushauri kutoka kwa watu wema.
5. Moja ya nyakati nzuri za Du’aa ni katika nyakati za kabla ya Alfajiri (Swalatu-Tahajjud)
6. Swalah ya Jamaa msikitini haswa alfajiri ni muhimu.
7. Kulia kwa sababu ya Allaah سبحانه وتعالى humkurubisha mtu zaidi kwa Allaah na humuongezea imani na mapenzi ya Allaah سبحانه وتعالى
8. Kusujudu sajdah ya kumshukuru Allaah سبحانه وتعالى kila unapopata au unaposikia jambo jema.
9. Kuweka Nia ya jambo jema Allaah سبحانه وتعالى Atakuonyesha njia.

Zifuatazo ni aya zenye kutufundisha faida ya Kutawakkal kwa Allaah, na kuwa Wacha Mungu.
(( وَمَن يَتَّقِ اللَّهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا))
{{Na anaye mcha Mwenyezi Mungu humtengezea njia ya kutokea}}
At-Twalaaq: 2
(( وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لاَ يَحْتَسِبُ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّهِ فَهُوَ حَسْبُهُ إِنَّ اللَّهَ بَالِغُ أَمْرِهِ قَدْ جَعَلَ اللَّهُ
لِكُلِّ شَيْءٍ قَدْرًا))
{{Na humruzuku kwa njia asiyotazamia. Na anayemtegemea Mwenyezi Mungu Yeye humtosha. Hakika Mwenyezi Mungu anatimiza amri yake. Mwenyezi Mungu kajaalia kila kitu na kipimo chake}} At-Talaaq: 3
(( وَمَن يَتَّقِ اللَّهَ يَجْعَل لَّهُ مِنْ أَمْرِهِ يُسْرًا ))
{{Na anaye mcha Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu humfanyia mambo yake kuwa mepesi}} At-Talaaq : 4
Allaahumma tujaalie tuwe wacha Mungu, wenye kutawakkal Kwako daima, Utusahilishie mambo yetu, na Uturuzuku kheri nyingi. Aamiin.

No comments: