بسم الله الرحمن الرحيم

kutafuta elimu ni faradhi kwa kila muislamu
الحمد لله الذي نستعينه ونستغفره ونعوذ بالله من شرور أنفسنا ومن سيئات أعمالنا من يهد الله فلا مضل له ومن يضلل فلا هادي له .



ونشهد أن لا إله إلا الله وحده لا شريك له ونشهد أن محمدا عبده ورسوله أرسله بالهدى ودين الحق ليظهره على الدين كله وكفى بالله شهيدا




Friday, February 5, 2010

SOMA UJIHESABU NAFSI YAKO

SOMA UJIHESABU NAFSI YAKO.

1.Jee, umemdhukuru Mola na umemshukuru wakati wa kuamka kutoka usingizini?

2.Jee, umesali leo Sala ya Alfajiri Msikitini?

3.Jee, umesoma leo nyiradi za Asubuhi?

4.Jee, umemuomba siku ya leo Mola wako akuruzuku riziki ya halali?

5.Jee, umemshukuru Mola juu ya neema ya kuwa wewe ni Mwislamu?

6.Jee, umemshukuru Mola juu ya neema ya kuwa amekupa masikio na macho na moyo?

7.Jee, umekifungua leo kitabu cha Mola (Qur-ani) ukasoma baadhi ya Aya zake?

8.Jee, umemnasihi/umenasihi kuhusu mambo ya dini?

9.Jee, umemuomba Mola akuingize Peponi?

10.Jee, umejikinga kwa Mwenyezi Mungu akuepushe na Moto?

11.Jee, leo umesali Sala zako zote Msikitini?

12.Jee, leo umemsalia Mtume S.A.W.?

13.Jee, leo umeamrisha mema na kukataza mabaya?

14.Jee, leo ulikuwa na khushuu katika Sala zako unajua unayoyasema?

15.Jee, umependa kwa ajili ya Mola na kuchukia kwa ajili ya Mola?

16.Jee, leo umemuomba Mola msamaha akusamehe madhambi yako?

17.Jee, umemuomba Mola athibiti moyo wako juu ya dini Yake?

18.Jee, leo umemtabasamia katika uso wa ndugu yako Mwislamu.

19.Jee, umeusafisha ulimi wako kutokana na uongo, na kusema watu na kusema maneno ya upuuzi?

20.Jee, umeusafisha moyo wako kutokana na maradhi ya hasad n.k.

21.Jee, umeuzoesha moyo wako tabia njema kutokana na subira, uchaMungu, huruma kumtegemea Mola na ikhlaasi?

22.Jee, umekumbuka mauti na kaburi na siku ya Kiyama?
“FAHASABUU KABLA ANTUHASIBUU”

Thursday, February 4, 2010

MAONI YENU YAHITAJIKA

بسم اللَّهِ الرحمن الرحيم.
الحمد لله والصلاة والسلام على رسول الله
TUNAWAKARIBISHA WAISLAMU WOTE NDANI NA NJE YA UDOMSA KUTOA MAONI YENU JUU YA TOVUTI YETU HII TULIYOIANZISHA
INSHHALLAH TUPO KWA AJILI YA KUYATEKELEZA NA KUFANYIA KAZI
BIIDHIN ALLAH
WAWEZA KUANDIKA BARUA PEPE KWA ANUANI ILIYO JUU YA TOVUTI AU KWA KATIBU
SULEIMAN ABDALLAH-
+225 712 008 227 AU +225 754 371 115.
WAWEZA PIA KUTUMA MAKALA KATIKA SOFT COPY NAYO TUTAJARIBU KUIRUSHA KATIKA TOVUTI HII.

SALAM ALAYKUM WARAHMATULLAH WABARKATUH

بسم الله الرحمن الرحيم
الحمد لله الذي نستعينه ونستغفره ونعوذ بالله من شرور أنفسنا ومن سيئات أعمالنا من يهد الله فلا مضل له ومن يضلل فلا هادي له .
ونشهد أن لا إله إلا الله وحده لا شريك له ونشهد أن محمدا عبده ورسوله أرسله بالهدى ودين الحق ليظهره على الدين كله وكفى بالله شهيدا

Assalam alaykum ndugu zangu katika iiman.
shukrani zote anastahiki ALLAH(sw) rehma na aamani zimfikie mtukufu wa darja nabii Muhammad(saw).
(يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ مِنْ نَفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالاً كَثِيراً وَنِسَاءً وَاتَّقُوا اللَّهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ إِنَّ اللَّهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيباً) (النساء:1)
(يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَقُولُوا قَوْلاً سَدِيداً يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَنْ يُطِعِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزاً عَظِيماً) (الأحزاب:70-71)
أما بـــعـــــد

Ama baada ya kumshukuru Jalali na kumtakia rehma Rasuuli,
nichukue fursa hii kuwatambulisha nafasi hii niliyoruzukiwa na allah kuutangaza uislamu haswa tovuti hii ya jumuiya ya wanafunzi wa kiislamu chuo kikuu Dodoma kama inavyo julikana UDOMSA yaani University of Dodoma Muslim Students Association.
Jumuya yetu inaundwa na wanafunzi wasomi wa chuo kikuu Dodoma.
Chuo chetu kinapatikana Mkoa wa Dodoma katikati ya Nchi ya Tanzania.Ilianzishwa rasmi mnamo mwaka 2007/08 kwa kuanza tu kwa chuo kikuu hiki.
Lengo letu ni kuwa pamoja na kukamilisha yale yahusianayo na uislamu na waislamu ndani na nje ya chuo kikuu Dodoma.Kutoa Elimu na kutafuta elimu huswa ya kiislamu katika mazingira ya chuoni na wanachuo wa UDOM.
Jumuiya hii inaundwa na idara ambazo zinapatikana katika College zote za University of Dodoma,Idara hizi ni
IDARA YA HABARI NA MAHUSIANO
IDARA YA ELIMU NA DAAWA
IDARA YA IMAMU NA MUDIR
IDARA YA FEDHA NA UCHUMI
IDARA YA MAKTABA.
Idara hizi husimamia utendaji wa malengo ya jumuiya na wanajumuiya kwa ujumla
Jumuiya ina mawasiliano na jumuiya za ndani nanje ya chuo.Waweza wasiliana nasi kwa anuani zifuatazo
UDOMSA,
IDARA YA HABARI NA MAHUSIANO,
BOX 1160,
DODOMA,TANZANIA
Mudir wa udomsa-+225715 960 706
Katibu Idara ya habari na Mahusiano udomsa-+225712 008 227/+225754371115
katibu mkuu udomsa-+225713160330/+225763 930 545